KANISA LA LAODEKIA

Kanisa la Laodekia ni kanisa la siku hizi za Mwisho. Ujumbe wa Kanisa la Laodekia unahusu wakristo wa kipindi chetu hasa wa kanisa la waadventista wasabato. Mimi na wewe tunaweza tukawa ni miongoni mwa wale ambao Yesu amewaongelea katika kanisa la Laodekia. Hivyo kila mmoja na ajitafakari mienendo yake na kama inaendana na tabia ya kanisa la Laodekia inabidi aachane nayo haraka asije akatapikwa kutoka katika kinywa cha Yesu. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. Nakupa shauri...