144,000 NI NANI?
Katika Kitabu cha ufunuo wa Yohana Sura ya saba tunaona kuwa kuna watu
ambao idadi yake ni 144000 ambao hao ndio washindi wa dhambi kipindi Yesu
anakuja tena kwa mara ya pili. Kwa vile watu hawa ambao wamefua mavazi yao na
kujiweka tayari na ambao wanatabia ya Kristo katika mienendo yao ya maisha na
kweli walioipokea ndio wanayoiishi kabla ya kuja kwake Yesu. Tunajua kuwa Watu
hawa 144,000 wanatoka katika wakati huu ambao tuliopo. Katika wakati tuliopo kutakuwa na aina mbili ya
waadventista wasabato ambao ni wa Kanisa la Fildefia na wa kanisa la Laodekia.
Wa kanisa la Fildefia ndio kanisa la Mungu ambao wanajulikana kama pia ni
144,000 ambao watatiwa Muhuri. Lakini kwa upande mwingine wa kanisa la Laodekia
ni waadventista wasabato ambao wanajua ukweli lakini hawaendi sawa sawa na huo
ukweli wakijiona kuwa hawana haja na kitu.
Nikasikia hesabu yao waliotiwa muhuri katika kila kabila ya Waisraeli, watu
mia na arobaini na nne elfu
(Ufunuo 7:4)Tunaona kuwa watu hawa ndio ambao watatiwa Muhuri wa Mungu katika paji la nyuso zao. Sasa kwa vile kanisa la waadventista wasabato lipo katika Hali ya Laodekia na uwepo wa Mungu haupo ndani yake,
Kanisa lipo katika hali ya Laodekia. Uwepo wa Mungu haupo
katikati yake.
(EGW, Last day
Events, 49.1)
Inamaana kuwa watu hawa Hawatoki katika kanisa la Laodekia bali wanatoka
katika kanisa la Filedefia.Hawa ni watu kutoka katika kanisa la Fildefia. Hili ndilo kanisa la kweli la Mungu katika kipindi
hichi cha siku za Mwisho. James White alisema kuwa kanisa la filedefia lilianza
mwaka 1844 ambao walikuwa ni watu wanaoangalia maandiko na kutafuta nuru ya
Kristo na watakuwepo mpaka Yesu atakaporudi tena. Yoyote ambaye anaishi sawa na neno la Yesu na sheria zake na kuakisi tabia ya Kristo ya upole na upendo anaahadi kuwa atatiwa muhuri nakuwa miongoni mwa hawa 144,000
Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo
yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye
kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye. Nayajua
matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana
awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala
hukulikana jina languTazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao
kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje
kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda. Kwa kuwa umelishika
neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa
iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi. Naja
upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. Yeye ashindaye,
nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena
kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu
wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina
langu mwenyewe, lile jipya. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo
Roho ayaambia makanisa.
(Ufunuo 3:7-13)
Tunagundua kitu hapa kuwa Kanisa la Filadelfia ni kanisa ambalo watu wake ni
waaminifu kwa Mungu na wametunza neno la Mungu. Kwa vile Biblia imesema kuwa "utoke
katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu
wakaao juu ya nchi" Tunajua kuwa kanisa hili lipo mpaka sasa na ni watu
ambao watashikilia imani yao kipindi cha majaribu. Watu wa Mungu ambao
watatetea imani zao mpaka kufa ndio watu wa kanisa la Filadelfia. Kwa maana hiyo watashinda majaribu ya shetani katika
kipindi hicho cha kujaribiwa ambacho muda sio mrefu kina kuja, watatiwa muhuri
wa Mungu kuwa ni washindi wa Dhambi. Ellen White alisema
“Unafikiri kuwa wale wanaoabudu katika miguu ya watakatifu (Ufunuo 3:9)
mwishoni wataokolewa. Hapa lazima nitofautiane na wewe, Kwa kuwa Mungu
amenionesha kuwa hawa ni kundi la wanaojiita waadventista ambao wameasi na
wamemsurubisha mwana wa Mungu upya, na kumuweka katika aibu ya wazi. Na katika
saa ya majaribu ambayo itakuja, kuonesha tabia halisi ya kila mtu, watajua kuwa
wamepotea milele na watajawa na sononeko rohoni, na watainama katika miguu ya
watakatifu” (EGW, A word
to the little Flock, p.g 12)
Tunaona kuwa Ellen White anasema wale ambao wataabudu katika miguu ya
watakatifu ni waadventista pia, lakini waadventista hawa ni wale ambao wameasi
kwa kutoenda sawa sawa na kweli ambazo Mungu ametoa. Hivyo tunaelewa kuwa
katika kanisa la waadventista wasabato kuna waadvetista wa kweli ambao ndio
Kanisa la Filedelfia na kuna kundi la wasabato wa uongo ambao ndio sinagogi la
Shetani au kwa jina lingine ni kanisa Laodekia lakini wapo humo humo kanisani wajiitao
wayahudi kumbe sio wayahudi maana yake ni kwamba wanajiita ni waadventista
wasabato lakini sio waadventista wasabato kweli. Sinagogi la shetani inaweza
ikawa ni washiriki, viongozi wa kanisa, wachungaji, viongozi wa General
conference n.k Lakini japokuwa na umaafuru wao na kuonekana kuwa ni watu wa
Mungu lakini ukweli ni kwamba hawa ni sinagogi la shetani. Sasa Kwa vile Ellen
White amesema kuwa Kanisa lipo katika hali ya Leodekia na uwepo wa Mungu haupo
katikati yake tunaelewa kuwa Sinagogi la shetani katika Kanisa la Filedelfia ni
waadventista wasabato ambao wanajua ukweli lakini hawaishi sawasawa na huo
ukweli wanaojulikana tena kama kanisa Laodekia.
Kuna ambao ni wasabato jina na kuna ambao ni wasabato wa kweli. Wasabato wa
kweli ndio watu wa Mungu waliopo katika kanisa la Fildefia na wasabato walioasi
kweli za Mungu ndio walio katika Kanisa la Laodekia ambao ni vuguvugu. Ellen White anasema
Hawa 144,000 wametiwa muhuri na wameungana kwa pamoja. Katika paji za nyuso
zao wameandikwa jina la Mungu, Yerusalem mpya na nyota yenye utukufu ambayo ina jina
jipya la Yesu. Katika Furaha yetu na katika hali yetu ya utakatifu waovu
walikasirishwa na wakafanya haraka Kunyanyua mikono yao ili watutupe gerezani,
Tuliponyoosha mikono yetu kwa jina la Yesu wakaanguka wakiwa hawana msaada
katika ardhi. Hivyo Sinagogi la Shetani walipoona kuwa Mungu anatupenda ambao
tunaoshana miguu sisi kwa sisi na kusalimiana kwa busu takatifu, na wakaabudu
katika miguu yetu
(EGW, Early Writtings, p.g 15).
Tunaona kuwa hawa watu 144,000 ni watu katika kanisa la Filedelfia kwa
maana sinagogi la Shetani limezungumziwa katika kanisa la Filedelfia. Hawa ndio
ambao watatiwa Muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao. Sasa kwa vile Ellen
White amesema kuwa sinagogi la shetani ni waadventista wasabato ambao hawaendeni
sawa na neno la Mungu, Tunaelewa kuwa kuna wakati utafika ambapo waadventista
wasabato watawasaliti waadventista wenzao. Kuwa ndani ya kanisa kuna wakati
utafika ambapo waadventista walioasi kweli za Mungu watakapo watesa na kuwaweka
gerezani waadventista wenzao ambao wanaamini na kushikilia katika kweli za
Biblia. Na wakati huo umekwishaanza kwa maana wapo wengi ambao wanafutiwa
ushirika kwa kuliambia kanisa la Laodekia makosa yake. Kwa hiyo mpaka sasa
tumejifunza nini
i.
Wanaojiita
waadventista au waadventista wasioenda sawa na Nuru zilizofunuliwa sio
waadventista kwa Mujibu wa Biblia.
ii.
Fildelfia
ndio kanisa la kweli la Mungu ambalo watu wa Mungu watapita katika saa ya
Majaribu au pia inajulikana kama taabu ya Yakobo.
iii.
Wanaojiita
waadventista au waadventista wasioenda sawa na kweli za Biblia hawa ndio
sinagogi la shetani au kwa jina lingine ndio kanisa la Laodekia.
Ukweli ndio huu ya kuwa Mungu anakanisa lake. Kanisa lake sio jengo au
dhehebu fulani bali kanisa la Yesu ni wale wanamuamini na kumuabudu Yesu katika
kweli na Roho. Kuna wengi ambao wanajua kweli za Biblia lakini hawana upendo na
hawana tabia ya Yesu. Kwa hiyo kila mmoja anatakiwa atambue kuwa kuwa mshiriki
wa kanisa la waadventista msabato haimaanishi kuwa unauhakika wa kutiwa Muhuri au kuurithi ufalme wa mbinguni.
Ellen White anasema
“Mungu anakanisa. Sio kanisa kubwa na wala sio kama taifa zima. Ni watu
wanaompenda Mungu na kutunza amri zake. Kwa kuwa walipo wawili watatu
wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao (Mathayo 18:20).
Pale ambapo Yesu yupo pamoja na wachache ambao ni wanyenyekevu, hilo ndio
kanisa la Yesu, Kwa maana uwepo wa juu wa yule mtakatifu anayeijaza milele,
pekee unaweza kutengeneza kanisa” (EGW, The upward look, p.315)
Mungu anakanisa lake na kanisa lake sio hili linaloonekana kwa macho, bali
ni lile kanisa ambalo limejengwa katika utii wa amri zake. Sisemi kuwa watu
wasiwe wanahudhuria ibada kanisani kwasababu kanisa la Mungu sio Dhehebu la waadventista wasabato, ila ukweli ni kwamba, kanisa la Mungu ni wale wanaolitii jina la
Bwana na kutunza na kuishi sawa sawa na Nuru zilizofunuliwa. Kanisa la
waadventista wasabato lenyewe linakiri kuwa ni kanisa Laodekia ambalo Mungu
hayupo tena katikati yake.
Leo tunasita kusema kuwa sisi ni kanisa masalia, Bali ni Laodekia, Hao ndio
sisi, sisi pekee yetu... Hakuna kikundi kingine cha kikristo kinaweza pingana
au kusita kutambua hilo... Bila kupingika Kanisa la waadventista wasabato ndio
kikundi kilichosemwa katika ujumbe wa siku za mwisho. (Adventist Review,
August 28,2008).
Kwa maana hiyo kanisa la waadentista wasabato linakiri kuwa ni Kanisa
Laodekia. Hivyo sio kanisa aminifu kwa Mungu tena. Kuna watu wa Mungu ambao ni waaminifu na
wanatunza imani ya waasisi wa kanisa. Kuna watu wa Mungu ndani ya kanisa na
wasabato ambao watatiwa muhuri watu hawa ni watu kutoka kanisa la fildefia. Mungu anafanya kazi na mtu mmoja mmoja ndani ya
kanisa la waadventista wasabato na sio tena kanisa kwa ujumla kama ilivyokuwa
hapo mwanzo. Baada ya kuwa kanisa la waadventista wasabato kuwa katika uasi,
Mungu hafanyi tena kazi na kanisa hili kama dhehebu bali uwepo wake utakuwa na wale wanaoakisi tabia ya Kristo katika maisha yao. Uwepo wa Mungu haupo katika dhehebu
hili kwasababu tayari ni vuguvugu. Bali uwepo wa Mungu upo kwa mmoja mmoja. Yesu alisema.
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua
mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.(Ufunuo 3:20).
Ujumbe huu wa Yesu upo katika kanisa la Laodekia katika kitabu cha ufunuo. Maana yake ni kwamba Yesu
anaalika mtu mmoja mmoja kumkubali katika moyo wake na kuwa moto badala ya kuwa
vuguvugu hata kama inamlazimu kupingana na kile kanisa inaamini. Yoyote ambaye atakubali kumfungulia Yesu moyo mwake, Yesu ataingia
na kumgeuza moyo wake na kumpeleka katika Nuru za Biblia ambazo wakati mwingine
zinapingana na kile ambacho kanisa linaamini kwa sasa. Watu hawa wa Mungu ndio
watakuwa katika kanisa la Fildelfia ambalo ndio kanisa la Mungu ambalo linapewa
Muhuri wa Mungu. Ndani ya kanisa la Wasabato kuwa watu wa Mungu na hao ndio
kanisa la Mungu na sio Dhehebu la waadventista wasabato.