KANISA LA LAODEKIA
Kanisa la Laodekia ni kanisa la
siku hizi za Mwisho. Ujumbe wa Kanisa la Laodekia unahusu wakristo wa kipindi
chetu hasa wa kanisa la waadventista wasabato. Mimi na wewe tunaweza
tukawa ni miongoni mwa wale ambao Yesu amewaongelea katika kanisa la Laodekia.
Hivyo kila mmoja na ajitafakari mienendo yake na kama inaendana na tabia
ya kanisa la Laodekia inabidi aachane nayo haraka asije akatapikwa
kutoka katika kinywa cha Yesu.
Na kwa malaika wa kanisa
lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye
mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Nayajua matendo
yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au
moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke
katika kinywa changu. Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala
sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na
maskini, na kipofu, na uchi. Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu
iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya
uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate
kuona. Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii,
ukatubu. Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu,
na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja
nami. Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha
enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake
cha enzi. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia
makanisa. (Ufunuo 3:14-22)
Tunaona kuwa hakuna sifa yoyote
nzuri ambayo imetamkwa na Yesu kuhusu kanisa la Laodekia. Bali anasema kuwa ni
kanisa ambalo sio moto wala sio baridi bali ni Vuguvugu. Tunajifunza nini hapa?
kwa Kawaida maji yaliyovuguvugu hapo mwanzo yalikuwa ya moto. Lakini
kadiri muda unavyoendelea kwenda maji hayo yanaanza kupoa na kufikia wakati
ambapo ni vuguvugu. Kwa maana hiyo kanisa la Laodekia hapo mwanzo
lilikuwa ni kanisa ambalo limeshikilia kweli za Biblia. Lakini kadiri muda
unavyoenda kanisa hili linaacha kweli zile za Biblia na kushikamana na Dunia.
Mafundisho ambayo hayatokani na biblia au kutoishi sawa sawa na biblia ndio
inafanya kuwepo na uvuguvugu katika kanisa hili. Pale ambapo Kanisa
linaacha kweli ya Biblia na kwenda katika njia zisizowekwa na Biblia,
tunatambua kuwa kuna uvuguvugu ule ambao umesemwa katika kanisa la Leodekia.
Sasa Tunaona kuwa Yesu anasema
kuwa kanisa hili atalitapika litoke katika mdomo wake. Maana yake ni kwamba
kanisa hili Yesu ataliacha lisiwe kanisa lake kama halitatubu na ataondoa
nafasi yake katika ufalme wa Mungu. Lakini swali linakuja Je kanisa hili la
Leodekia linakubali makosa yake? Kitu cha ajabu ni kwamba kanisa hili linaona
lenyewe halina mapungufu yoyote kwa maana linaona ni tajiri na limejitajirisha
na wala halina shida na kitu chochote kile. Utajiri unaozungumziwa hapa ni
utajiri wa mambo ya kiroho. Linajivunia utajiri wa kiroho, na kiburi chake
kinaonekana wazi kwa maana Linasema halina haja na kitu. Maana yake ni kwamba
Kama ni Biblia, linaona linaijua Biblia kiasi ambacho halina haja na kitu
chochote kipya. Kama ni Kweli za Biblia, kanisa hili linaona Linajua kweli zote
za Biblia kiasi ambacho halina haja na Kitu. Kama ni Kumjua Yesu, kanisa hili
linaona linamjua Yesu mno kiasi cha kwamba halina haya na kitu chochote kile.
Lakini Jinsi kanisa hili la Laodekia linavyojiona, ni tofauti kabisa na jinsi
Yesu anavyoliona. Yesu akiliangalia kanisa hili anaona kuwa ni kanisa nyonge,
lenye mashaka, na kipofu na lipo uchi. Japokuwa na mapungufu haja lakini kanisa
Leodekia linaona kuwa ni tajiri na limejitajirisha mno. Kanisa Leodekia
halitaki Kujifunza chochote kipya wala kuambiwa makosa yake. Hivyo kwa ufupi
Tunaona wazi kuwa Kanisa la Laodekia hapo mwanzo lilikuwa ni kanisa Ambalo ni
jema na lenye Ukweli mwingi wa Biblia likiwa limejiweka katika unyenyekevu na utayari wa kujifunza mambo mapya, lakini Limebadilika na kuwa ni kanisa
lisilofaa kwa maana limegeuka na kuwa ni kanisa lililoasi likichanganya
mafundisho ya ukweli na uongo na kuwa na kiburi cha kutotaka kusikia neno lolote jipya. Unabii huu wa kanisa la Laodekia unafanana sana
na ule wa nabii Isaya.
"Mji huu uliokuwa mwaminifu umekuwaje kahaba! Yeye aliyejaa hukumu ya haki; haki ilikaa ndani yake, bali sasa wauaji! Fedha yako imekuwa takataka, divai yako imechanganywa na maji. Wakuu wako ni waasi, na rafiki za wevi; kila mtu hupenda rushwa, hufuata malipo; hawampatii yatima haki yake, wala maneno ya mjane hayawawasilii". (Isaya 1:21-23)
Mji mtakatifu unaosemwa na isaya ni kanisa la Mungu, na kanisa la siku hizi za Mwisho ni kanisa la Laodekia. Kwa maana hapo mwanzo kanisa Laodekia lilikuwa ni kanisa aminifu tena nyenyekevu lakini sasa limegeuka na kuwa ni kanisa ambalo limepotoka likichanganya mafundisho ya ukweli na uongo au kushindwa kuishi sawa sawa na Nuru zilizofunuliwa. Kutokana na hili, kanisa hili linatapikwa kutoka katika kinywa cha Yesu. Unabii wa kanisa Laodekia unalihusu kanisa la waadventista wasabato kwa kiwango kikubwa sana ambalo walipata nuru nyingi za Biblia na kuujua ukweli, lakini sasa haliishi sawa sawa na Nuru hizo ambazo Yesu alizitoa. Lakini sio rahisi Kanisa la Waadvetista wasabato kujiona lina makosa au kukubali kuwa msingi Fulani wa Kanisa au Miongozo na katiba ya Kanisa kuwa inamakosa kwasababu ya kiburi. Kwasababu linaamini kuwa limekamilika na halina makosa.Mara nyingi Kanisa linaona kuwa taratibu zake hazina makosa na kila mmoja ambaye ni mshiriki wa Kanisa la Waadventista wasabato atakubaliana na mimi kuwa ni mara nyingi sana tunaambiwa kuwa kanisa la wasabato ndio kanisa lenye kweli zote za biblia yaani ni kanisa lenye utajiri wa mambo ya kiroho, lakini ukweli huo hauna faida kama haubadili matendo yetu kumuakisi Yesu.Ellen White anasema
"Udunia hautakiwi uingizwe
katika Kanisa, na kuoana na kanisa, na kufanya umoja nao. Kwa jinsi hii kanisa
linakuwa limeasi kama jinsi ilivyoelezwa katika Ufunuo wa Yohana
"Ngome ya kila ndege mchafu na mwenye kuchukiza"(Testimonies
to Ministers, 265.1)
Ni kanisa gani Ellen White
analisemea hapa? Ni kanisa la waadventista wasabato. Anaongea na wasabato waliondani ya kanisa. Pale ambapo Udunia unaanza
kuingia katika kanisa, ni kiashiria kuwa uasi umeanza kuingia katika kanisa.
Udunia unaonekana katika mavazi, Katika maongezi na katika mitindo mbalimbali ya maisha.
Kwahiyo ndani ya kanisa la waadventista wasabato kama udunia
umeingia katika kanisa maana yake ni kwamba ule uasi umengia na kufanya kanisa
liwe katika uvuguvugu.
Kristo alipoona wayahudi
kama taifa wameachana na Mungu, aliona pia Kanisa la Kristo linaungana na
ulimwengu na upapa, itambidi kusema na wale ambao walikuwa na nuru kubwa
na maarifa mengi,kama alivyosema na wayahudi, " Laiti ungalijua, hata
wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako"(EGW,Kress
Collection 153.3)
Ni nani ambao walipewa nuru
kubwa na maarifa mengi? Ni kanisa la waadventista wasabato. Katika Nukuu hii
unaona kuwa Kama Kristo alivyoliacha Wayahudi waliomkataa ndiyo atakavyoliacha
kanisa lake ambalo nalo limemuacha na kuongozana na Upapa na mambo ya
dunia.Kama Kanisa linamuacha Kristo na kufatana na dunia na mafundisho ya upapa, Kristo hawezi kuwepo
katika kanisa hilo. Makanisa ya kikristo yanaungana na upapa katika
mafundisho. Kama Katika kanisa kuna mafundisho ya upapa ni wazi kuwa Yesu
Kristo hawezi kukaa hapo mpaka kufanyike matengenezo ya kuachana na mafundisho
hayo. Lakini kitu cha ajabu ni kwamba kanisa la Laodekia halioni kosa lake
katika mafundisho yake. Kanisa la Laodekia Lina mkataa Kristo pamoja na haki yake kwa kushikilia mafundisho ya upapa.
Tunaendelea kuona kuwa kadiri muda unavyoenda Kanisa la Waadventista wasabato
linaendelea kulegeza misimamo yake katika mavazi, katika ibada, na katika
kutengana na udunia na upapa. Japokuwa hili linaweza likaonekana ni sahihi mbele za
wanadamu lakini halipo sawa mbele za Mungu.
Bwana Yesu ataendelea kuwa na
watu wake aliowachagua kumtumikia. Wayahudi walipomkataaYesu, Mfalme wa uhai,
aliuchukua ufalme wa Mungu utoke kwao na kuwapa watu wa mataifa. Mungu
ataendelea kufanya kazi katika kanuni hii na kila tawi la kazi yake. Pale
kanisa linapothibitishwa sio aminifu wenye neno la Bwana, bila kuangalia nafasi
yao ilikuwaje, kuwa muito wao ni mkuu na mtukufu, Bwana hawezi tena kufanya
kazi nao. Watu wengine watachaguliwa, kuchukua majikumu muhimu.
(EGW, UL 131.3)
Je ni kanisa gani Ellen White analolimaanishia hapa? Hakuna kanisa lingine isipokuwa kanisa la Waadventista wasabato. Tunaona kuwa Yesu kristo anaangalia kwa kiasi gani kanisa ni aminifu katika Neno la Bwana. Kanisa la waadventista wasabato lilichaguliwa ili litangazie ulimwengu ujio wa Yesu mara ya pili. Yesu aliliinua na kulipa sabato kama ishara kati ya Mungu na kanisa lake. Lakini japokuwa nafasi yao ilikuwa ni kubwa na ya juu. Kwa vile limegeuka sasa na kuwa ni vuguvugu, tunajua kuwa uwepo wa Mungu haupo tena katika kanisa.
Wale ambao wanajisifu katika
Nuru zao, na bado wanashindwa kutembea katika njia hiyo, Yesu anasema
"Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu
zake kuliko ninyi. Nawe Kapernaumu,[Kanisa la waadventista wasabato ambao
walikuwa na nuru kubwa] Ulitukuzwa hata mbinguni [Katika nafasi ya
heshima] Utashushwa hata kuzimu: kama kazi iliyofanyika kwako
ingelifanyika kwa Sodoma, ingelibakia mpaka hivi leo. (Review
and Herald August 1, 1893) Maneno katika mabano yaliwekwa na Ellen White
mwenyewe.
Tunaona kuwa Ellen White
mwenyewe anasema wazi kuwa kanisa la waadventista wasabato ambao walipewa nuru
kubwa linajisifu idadi ya Nuru walizo nazo lakini hawaendi sawa sawa na kweli
hizo au nuru hizo, kuwa watashushwa hata kuzimu yani Yesu ataliacha kanisa lake
la waadventista wasabato kwa maana linashindwa kutembea sawa sawa na Nuru hizo.
Kanisa la waadventista wasabato linajisifu kuwa ndio kanisa pekee linalotunza
sabato ya Kweli katika Biblia nani kweli kuwa sabato ni Jumamosi siku ya saba
ya juma, Lakini linashindwa kwenda sawa na nuru zile ambazo Yesu alilipatia,
kama jinsi sahihi ya kutunza sabato. Mpaka hapa tulipofika Ellen White
anatusaidia kugundua kuwa Kanisa Leodekia linahusu Kanisa la waadventista
wasabato kwa. Ambalo linajivunia Nuru walizonazo lakini hawaendi sawa na Nuru hizo.
Ujumbe kwa kanisa la
Laodekia unahusu hali zetu. Jinsi gani ilivyowazi kwa wale wanaofikiri kuwa
wanaukweli wote, wakiwa na kiburi katika maarifa ya neno la Mungu, wakati nguvu
yake inayotakasa haipo katika maisha yao.Nguvu ya upendo wa Mungu imepungua
katika mioyo yao, Lakini nguvu hii ya upendo ndio inawafanya watu wa Mungu nuru
ya ulimwengu (EGW 1Selected Messages 357.1)
Je nguvu ya upendo kati ya mtu
na mtu imepungua sana katika kanisa, Upendo wa kindugu umepungua sana. Lakini
japokuwa upendo umepungua hivi bado tunajivunia kuwa tunajua kweli za
neno la Mungu wakati upendo wa Mungu na haki yake haimo moyoni mwetu. Tunasema
tunamjua Mungu wakati mioyo yetu ni migumu sana kumsaidia mwenye shida,
Tunasema tunajua nuru za neno la Kristo wakati ukweli huo hatujauruhusu ufanye
utakaso mioyoni kwetu. Tunapoyaona hayo yote jua kuwa Ujumbe wa kanisa la
Laodekia unahusu hali zetu sisi kama waadventista wasabato. Uwepo wa Mungu
haupo kati yetu.
Ujumbe kwa kanisa la Laodekia
unahusu waadventista wasabato ambao walikuwa na nuru kubwa na
hawajatembea katika Nuru. Ni wale ambao walifanya taaluma kubwa, lakini
hawakutunza hatua zao na kiongozi wao. Watatemwa watoke katika kinywa cha Mungu
kama hawatatubu. (EGW, 2Selected Messages 66.2)
Ellen White amesema wazi kuwa
ujumbe wa kanisa la Laodekia unahusu waadventista wasabato. Hili ni onyo la
kila mmoja aliyendani ya kanisa la waadventista wasabato. Ndani ya kanisa la
waadventista wasabato kuna wengi ambao wanajua ukweli wenda wanaweza kuwa
ni wachungaji, wazee wa kanisa, mashemasi, raisi wa General conference na
viongozi wengine wengi na washiriki, lakini japokuwa wanajua ukweli huo,
Hawaendi sawa sawa na Kweli hiyo, Yesu anasema kuwa waadventista hawa watatemwa
watoke katika kinywa chake kama hawatabadili mienendo yao mibaya. Lakini Je
watu hawa watatubu? kwa maana kanisa la Laodekia linaona ni tajiri na halina
shida na kitu.
Hali ya kanisa inayowakilishwa
na wale mabikira wapumbavu pia inaongelewa kama hali ya Laodekia. Shahidi wa
Kweli anasema Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa
heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu
baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Kwa kuwa wasema,
Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa
wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi
(EGW, Review and Herald 19,1890)
Mtumishi wa Mungu Ellen White
anasema kuwa wale mabirika watano wapumbavu ambao taa zao hazikuwa na mafuta
ndio hali halisi ya kanisa la Laodekia. Kwa vile Ellen White anaona hali ya
kanisa la waadventista wasabato inayofananishwa na wale mabikira watano ndio
hali ile ile anayoiona katika kanisa la Laodekia, tunajua kuwa Kanisa la
waadventista wasabato lisipofanya matengenezo litatapikwa litoke katika kinywa
cha Yesu. Ellen White anazungumza na kanisa la waadventista wasabato akisema
"Tusifikirie kuwa tuna
kweli zote, kwamba tunaelewa nguzo kuu za Imani yetu, na kutulia
katika ufahamu huu, Ukweli ni ukweli endelevu lazima tutembee katika Nuru
iliyoongezeka" (EGW, CW 33.2)
Mara nyingi sana kanisa linaamini kuwa lina nuru zote za Biblia na kutulia hapo, hili limekuwa ndio kiburi kikubwa cha kanisa la waadventista wasabato. Lakini Ellen White amesema wazi kuwa tusifikirie hata kidogo kuwa tuna Kweli zote,maana yake ni kwamba sio kweli kuwa tunakweli zote. Yoyote anayesema kuwa tuna kweli zote anaongea uongo na anafanya watu wasijisumbue kutafuta kweli katika biblia. Amesema wazi kuwa kweli za Biblia huwa ni endelevu. Kanisa letu la waadventista wasabato kama jinsi lilivyo kanisa la Laodekia linadhania kuwa linakweli zote za Biblia na kuridhika jambo ambalo kwa maelezo ya Ellen White sio kweli. Sasa tuangalie ushauri wa Yesu kwa Kanisa la Laodekia ni nini?Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. Yesu ameliambia Kanisa la Laodekia linunue kwake dhahabu iliyosafishwa kwa Moto, Lakini Dhahabu hii iliyosafishwa kwa moto maana yake ni nini? Ellen White anasema
"Dhahabu iliyotajwa na Kristo,
shahidi wa kweli, ambayo wote tunatakiwa tuwenayo, imeoneshwa kwangu kwamba ni
Kuwa katika Imani na upendo kwa ujumla, na upendo unaoweka mbele Imani"(
2T 36.2)
Tunaelewa kuwa Yesu aliposema
kanisa la Laodekia linunue kwake Dhahabu iliyosafishwa maana yake ni kwamba
kanisa la Laodekia lichukue kwake Imani na upendo ule ambao Yesu mwenyewe
alikuwa nao. Ni kweli kuwa katika kanisa la Waadventista wasabato upendo umepoa
sana kwahiyo Yesu analiambia kuwa linunue kwake upendo na Imani. Yesu pia
analipa ushauri kanisa La laodekia kuwa linunue kwake mavazi meupe mavazi meupe
yanayozungumziwa hapa ni haki ya Kristo. Kwahiyo Yesu anataka kanisa la
Laodekia livae haki yake ili lisiwe uchi. Pia anazungumzia kuhusu dawa ya macho
maana yake ni Kuwa na utambuzi wa mambo ya kiroho. Kwa maana nyingine ni kwamba
Kanisa la Laodekia Halina haki ya Kristo, Halina Imani na upendo wala halina
Utambuzi wa mambo ya kiroho. Sasa Je uwepo wa Mungu upo katika kanisa la
Waadventista wasabato baada ya kuona kuwa limegeuka na kuwa Laodekia?
Ellen White anasema
Kanisa lipo katika hali ya
Laodekia. Uwepo wa Mungu haupo katikati yake. (EGW Last
day Events, 49.1)
Japokuwa inawezekana ikawa ni
Ngumu kuamini, lakini Ellen White amesema wazi kuwa uwepo wa Mungu haupotena na
kanisa la waadventista wasabato kwasababu limegeuka na kuwa Kanisa la Laodekia