1YOHANA 5:8 NA MATHAYO 28:19 ZINASEMAJE?

1. 1YOHANA 5:8 " Kwa maana wako watatu washuhudiao Mbinguni Baba na neno na roho mtakatifu na watatu hawa ni umoja" (1yohana 5:8) Kwa kuanza kabisa, mstari huu ni mstari maarufu sana na unatumiwa kama ndio mstari mkuu unaoonesha kuthibitisha kuwa Mungu ni nafsi tatu. Lakini kwa mtu yoyote yule ambaye ni mwaminifu wa moyo na moyo wake hauna mabishano atajiuliza kwanini katika Mistari mingi ya Biblia Mungu mwenyewe anashuhudia kuwa yeye ni nafsi moja afu mstari mmoja huu ndio ubadili maana nzima ya Mungu mwenyewe? Na kuna watu japokuwa umetoa mistari mingi ya biblia kuonesha kuwa Mungu ni mmoja lakini bado anatumia mstari huu kutokukubali ukweli wa biblia hata kuifumbia macho mistari ya wazi inayoonesha kuwa Mungu ni nafsi moja tu. Sasa taratibu na tuangalie mstari huu kwa kina. Katika mstari huu msomaji na angalie vizuri. Je katika mstari huu wapi panaposema Mungu ni nafsi tatu? Au wapi panaposema kuwa Baba, mwana na Roho ni nafsi tatu za Mungu? Hata we...